Upside Down :Gari la rais Uhuru lambeba nambari ya usajili ikiwa imewekwa upande wa juu chini

Uhuru 's car 1 (1) (1)
Uhuru 's car 1 (1) (1)
Rais Uhuru Kenyatta aliwasili katika Jumba la Harambee katika gari ambalo nambari yake ya usajili iliweka juu chini.

Rais alikuwa amengojewa na  mawaziri kadhaa ili kutoa taarifa kuhusu  virusi vya Corona ambapo alithibitishwa kugunduliwa kwa visa viwili zaidi vya ugonjwa huo baada ya kisa cha kwanza kuripotiwa tarehe 13 machi . Gari hilo lililombeba rais  halikuwa bdenera maalum ya rais  au  bendera ya taifa na pia  Uhuru hakuwa na msaidizi ambaye huwa nyuma yake . Wakati wa hafla hiyo rais alitangaza mikakati kadhaa iliyochukuliwa na  serikali kuzuia maambukizi zaidi ya virusi hivyo ikiwemo kufungwa kwa shule zote .

Serikali pia imepiga marufuku kuingia nchini kwa raia wa kigeni kutoka nchi zilizoripoti visa vya Corona .Wakenya na raia wa kigeni wanaotaka kuja  nchini watahitajika kujitenga kwanza kwa siku nne au katika vituo vya afya vya umma  .Serikali pia imewaagiza wakenya kupeuka  Mikutano ya hadhara ,hafla za makanisa  na maeneo yenye watu wengi kwa siku 30 zijazo . Biashara ,kampuni za kibinafsi na mashirika ya umma pia zimeagizwa kuwaruhusu wafanyikazi wao kufanyia kazi nyumbani isipokuwa wale wanaofanya kazi zinazowahitaji kwenda afisini .

Rais Uhuru Kenyatta pia amewarai wakenya kutotumiapesa taslimu kufanya ununuzi bali kuzingatia kutumia mifumo ya malipo ya kutumia simu au kadi . Hospitali na duka za jumla zimetakiwa kutoa maji na sabuni kwa wateja ili waweze kuosha  mikono yao.