Rais wa shirikisho la soka barani afrika Ahmad Ahmad, ameachiliwa huru nchini Ufaransa bila kufunguliwa mashtaka yoyote baada ya kuhojiwa huko Marseille ,mwendesha mashtaka mjini humo amesema .
Xavier Tarabeux amesema Ahmad, aliyekuwa nchini Ufaransa kwa mkutano wa Fifa uliofanyika siku ya jumatano alihojiwa katika sehemu ya uchunguzi kuhusu ufisadi na ulagjai wa kughushi stakabadhi .