Rais wa zamani wa Congo Yhombi-Opango afariki baada ya kuambukizwa virusi vya Covid-19

opango
opango
Rais wa zamani wa   Jamhuri ya Congo Jacques Joaquim Yhombi-Opango,  amefariki jijini Paris   baada ya kupatikana na virusi vya Corona .

Alikuwa na umri wa miaka 81. Familia yake imesema alikuwa  akiugua hata kabla ya kupatikana na virusi vya corona .

Yhombi-Opango  aliongoza  Congo-Brazzaville  kutoka mwaka wa 1977 hadi mwaka wa 1979 alipoondolewa madarakani  na rais wa sasa wa taifa hilo   Denis Sassou Nguesso.  Aliwekwa jela kwa miaka kadhaa kabla ya  kuanzishwa kwa siasa za vyama vingi mwaka wa 1991 alipohudumu kama waziri mkuu kisha baadaye vita vya wenyewe kwa wenyewe vikazuka mwaka wa 1997. Alikimbilia mafichoni nchini Ufaransa  kabla ya kuruhusiwa kurejea nyumbani miaka 10 baadaye .