Rayvanny adaiwa kuiba idea ya wimbo wake Willy Paul

Msanii wa nyimbo za injili na mwenye utata Willy Paul amechapisha kipande cha video akionekana kulalamika kuwa mwenzake wa Tanzania Rayvanny kamwibia idea ya nyimbo yake Chuchuma. Nyimbo hii haijaweza kurekodiwa beat zinakwenda sawa.

Kulingana na Pozze, mipango ilikuwepo ya kuzama studio na kufanya bonge la collabo ila mambo yakashindikana. Katika Insta story yake staa Rayvanny anaonekana akiuimba muziki huo wa chuchuma na kuandika caption kuwa akiingia studio anadondosha hits tu.

Tumekusogezea hapa:

Willy Paul alifanya ngoma na staa huyu wa Tanzania muda mchache uliopita. Nyimbo hii inayofahamika kama Mmh inatamba na kufanya vizuri katika mtandao wa Youtube na upigwaji mkubwa katika redio na runinga mbalimbali.

Ushikaji wa dogo hawa wawili unaonekana haupo tena baada ya madai haya ya wizi wa nyimbo. Katika kipande hicho cha video, Willy Poze anaonekana akipiga mistari ya kikwake akitaja baadhi ya mastaa hapa nchini.

Msanii Rayvanny hajaweza kujibu madai hayo ya kuifanya ngoma yake Pozze.