Serikali ya Uingereza imewaonya raia wake dhidi ya kuja nchini Kenya kwa sababu ‘magaidi wanaweza kutekeleza mashambulizi’.Raia wa Uingereza wanaokuja Kenya wametakiwa kuwa waangalifu wakizuru maeneo ambayo watalii huyapenda kama vile hoteli ,mikahawa ,maduka ya jumla ,vilabu vya usiku na majengo ya kibiashara yenye shughuli nyingi. Maeneo ya kuabudu kama vile makanisa na miskiti pia yanaweza kulengwa . Ilani hiyo imezitaja kaunti za kaskazini mashariki kama vile Garissa na mandera na baadhi ya maeneo ya Tana River na Lamu kama sehemu ambazo raia wa Uingereza hawafai kwenda iwapo ziara hizo sio muhimu .
Ilani hiyo ya usafiri ambayo ilitolewa jumamosi haijazihusisha ziara za watali mbugani na maeno ya fuo za bahari pwani . Visiwa vya lamu na Manda pia vimeachw anje ya tahadhari hiyo . Kulingana na afisini ya FCO ambayo hutoa ilani hizo ,takriban wakaazi 190,000 wa Uingereza huzuru Kenya bila kupata matatizo yoyote. Ilani hiyo inajiri wiki moja baada ya magaidi kushambulia kambi ya kijeshi ya manda-magogoni inayotumiwa na wanajeshi wa Kenya na Marekani huko Lamu . Shambulizi hilo lilitishia kuvuruga mojawapo ya vitega uchumi muhimu sana kwa Kenya –Utalii kwa sababu ya wageni wengi wa kutoka mataifa ya nje ambao huzuru pwani ya Kenya .