Nyota huyo mwenye umri wa miaka 31 ambaye jina lake halisi ni Robyn Rihanna Fenty, ana mali yenye thamani ya Dola milioni 600 kulingana na Forbes –na kumpiku Madonna kwa dola milioni 30 ,Dion kwa pauni milioni 150 na Beyonce kwa dola milioni 200 .
Rihanna ambaye anafahamika sana kwa nyimbo zake tajika kama vile "Umbrella," "Diamonds" na "What's My Name?," hajapata mali yake kupitia muziki pekee .
Kulingana na Forbes pesa zake nyingi zimetokana na ushirikiano wake na kampuni ya Ufaransa ya LVMH ambayo hutengeza bidhaa za mvuto na vipodozi zenye majina mazito kama vile Christian Dior, Givenchy na Louis Vuitton.
Mwezi uliopita ,staa huyo wa Barbados alizindua leb yake ya fashoni Fenty katika mji wa Paris na kuwa mwanamke wa kwanza meusi kuunda nembo halisi kwa ushirikiano na LVMH.
Fenty ndio biashara ya hivi punde ya Rihanna baada ya kuzindua nyingine kama vile Savage X Fenty, mwaka jana na Fenty Beauty ya kuunda vipodozi mwaka wa 2017
Biashara hiyo ya nguo ndio yake ya kwanza katika soko la mavazi ya kifahari ingawaje amekuwa akiwatengezea nguo za kisasa wateja wa Uingereza kama vile River Island na alitangazwa kuwa mkurugenzi wa Ubunifu wa Puma mwaka wa 2014 .
Miradi mingine ya biashara za Rihanna imesifiwa kwa uwezo wa kuwashirikusha watu mbali mbali na matabaki tofauti . kampuni yake ya vipodozi ,imeunda aina 40 ya rangi ilahli ile inayotengeza nguo za ndani ina aina nyingi zinazoambatana na maoumbo tofauti ya watu . kampuni yake ya fashoni inamudu hata wanawake wenye kiwango cha size 14 (Marekani)