Aliyekuwa rais wa kilabu ya soka ya Real Madrid Lorenzo Sanz aliaga dunia siku ya jumamosi baada ya kulazwa hospitalini akiugua virusi vya Corona .
Sanz mwenye umri wa miaka 76 alikuwa rais wa kilabu hiyo ya Bernabeu kutoka 1995-2000, kipindi ambacho Real Madrid ilishinda kombe la mabingwa mara mbili .
" Babangu ameaga dunia ‘ aliandika mwanawe Sanz Lorenzo Sanz Duran katika Twitter .
" hakustahili kufika mwisho katika hali hii . mmoja wapo ya watu wajasiri na wenye bidii ambaye nimewahi kuwaona katika maisha yangu .Familia yake na kilabu ya Real Madrid ni vitu alivyovipenda sana’
Sanz aliwasajili wachezaji kama vile Roberto Carlos , Clarence Seedorf na Davor Suker wakati wa hatamu yake .