Ruto akutana na rafikiye baada ya miaka 35!

Naibu rais William Ruto hangeficvha furaha yake baada ya kukutana na jamaa waliokuwa wakisoma naye, Sospeter Ojwang.

Maraifiki hao wawili, walikutaona tena katika eneo la Lwanda siku ya Ijumaa kwa mara ya kwanza tangu walipofanya mtihani wa kidato cha nne katika shule ya Wareng.

"Delighted to meet and reunite with Sospeter Ojuwang, a former schoolmate at Wareng High School, Eldoret during my visit to Luanda, Vihiga County," Ruto aliandika kwenye twitter.

Ruto amabye alionekana mwenye furaha afanya mazungumzo ya kufana na rafiki huyo wake wa zamani na amabi alingana naye kwa jukwaa kuu.

"Tulikumbushana matukio ya siku zetu za ujana, tulicheka pamoja na kumtakia heri njema," Ruto alisema.

Wakenya walichangia kupitia mitandao ya kijamii baada ya picha za wawili hao kuchipuka. Kulingana na oicha Ruto alionekana barubaru huku rafiki yake akionekana mzee sana.

"Pesa ni lotion my friends, spot the difference, loosely translating to, money is like fine body lotion my friends, spot the difference," Frank Kiptoo aliandika kwenye twitter.

Baadhi ya wananchi nao walimtaka Ruto kumsaidia rafikiye kwa kumtafutia kazi.