Sababu za kumfukuza DK Kwenye Beat kutoka kwa wimbo wa msamaha - Guardian Angel

Guardian Angel hakuweza kumshirikisha msanii DK Kwenye Beat katika wimbo wake wa kuomba msamaha 'mercy' kwa sababu ya ukosoaji wa mashabiki katika mitandao wa kijamii.
"DK Kwenye Beat anapaswa kuwa na upatanisho na watu kwanza." Guardian Angel alizungumza katika mahojiano.

Mwezi mmoja ambao umepita msanii DK Kwenye Beat na msanii Hopekid waliweza kutuhumiwa na mwanamke mmoja kwa kuwa na ngono na yeye, kisha kumuambukiza maambukizi ya zinaa (S3xually transmitted Infection).

Ni jambo liliweza kuwafanya mashabiki na wananchi kuchangia huku wengi wakiwashtumu kwa kitendo hicho ambacho nichakusikitisha.

Ni jambo ambalo lilikuwa katika mstari wa mbele katika vyombo vingi vya habari, na watu wengi kuwakemea na kuwashtumu wasanii wa nyimbo za injili.

DK hajawahi omba msamaha hadharani, wala kuchukua hatua ya kumuomba mwanamke huyo msamaha kwa kile alifanya, msanii Guardian Angel alisema kuwa hataki watu na mashabiki waone kuwa anaunga mkono kwa kitendo ambacho DK alifanya.

Msanii huyo alishikwa na kuenda rumande kwa siku kadhaa, wengi wakimtetea na wengi wakimshtumu.

"Sitaki kuwa katika utata ata hivyo niliweza kuucheza na kurekodi wimbo huo upya tena ." Aliongea Guardian Angel.

Wiki iliyopita msanii Bahati aliweza kupata kukosolewa katika mtandao wake wa kijamii baada ya kumshirikisha DK Kwenye Beat katika wimbo wake wa kuomba msamaha.

Bahati aliweza kujitetea na kusema kuwa alikuwa anamsaidia ndugu yake DK kuomba msamaha kwa yale alitenda "I was helping my brother say sorry".

Katika wimbo wao ambao uko katika mtandao wa kijamii ya Youtube, watu wameweza kutoa maoni mabaya kuhusu kashfa ambayo msanii DK iliweza kumkumba.