Maneja wa wa msichana mwanasarakasi mwenye umri wa miaka 14 Wendy Waeni huenda akajipata katika mgogoro wa kisheria na baada ya maseneta Johnson Sakaja na Mutula Kilonzo Junior kujitolea kumsaidia mtoto huyo kuthibitisha madai yake dhidi ya maneja huyo Joe Mwangi .
Kupitia mazungumzo ya Twitter Viongozi hao wawili wamesema madai dhidi ya Mwangi yana vitendo vya uhalifu na pia yameibuka wakati viongozi wengine walipotoa ushahidi kwamba huenda Mwangi alikuwa akimtumia vibaya mtoto huyo kwa kuzifuja pesa zake .
Waeni amekuwa akifanya maigizo ndani na nje ya nchi na kutangamana na watu mashuhuri . Maisha yake hata hivyo hayajaboreka kwani yungali anaishi katika mtaa wa Huruma hapa jijini pamoja na mamake.