Sauti Sol tena !,wajumuishwa katika video ya Queen Sono

SAUTI
SAUTI

NA NICKSON TOSI

Waimbaji wa wimbo wa Suzzana  Sauti Sol aliingia katika rekodi baada ya kutoa wimbo utakaotumika katika filamu ya kwanza ya Afrika itakayotumika katika itakayoonyeshwa katika television Netflix kwa jina  “Queen Sono”.

Alihamisi wasanii hao wa kenya wa mitindo ya  afro-pop walikuwa Afrika Kusini katika uzinduzi wa filamu hiyo ya  Queen Sono,ambapo walitangaza wazi kuwa wao ndio walioimba wimbo utakaotumika katika filamu hiyo wakiwashirikisha wasanii  Sho Madjozi na  Black motion  kutokea Afrika Kusini.

“HISTORY! ✊🏿-- This is 's first African original and we're on the official soundtrack w/  &  . Cc   ,” Ulisoma ujumbe wa Sauti Sol.

Queen Sono ni filamu ya Afrika kusini inayoangazia maswala ya visa vya ugaidi na iliyoandaliwa na Kagiso Lediga na itaanza kuonyeshwa kwenye Netflix kuanzia Februari 28,2020.

Watakao shirika katika filamu hiyo ni, Pearl Thusi, Vuyo Dabula, Sechaba Morojele, Chi Mhende, Loyiso Madinga, Rob Van Vuuren, Kate Liquorish, Khathu Ramabulana, Enhle Maphumulo, Abigail Kubeka, Connie Chiume, Otto Nobela and James Ngcobo.

Katika filamu hiyo, Pearl Thusi [Quantico]mwana mitindo na mtangazaji wa televisheni anaigiza kama afisa wa ujasusi katika k8itengo cha ujasusi cha Afrika Kusini,na ambaye anatumia milango ya nyuma kupata kazi hiyo.

Queen Sono inasemekana kuwa itafunguwa milango ya filamu za kiafrika katika mataifa mengine kutokana na weledi wa waigizaji walioshirikishwa katika filamu hiyo wako nao.