Senate yapiga marufuku mikutano ya kamati kuzuia maambukizi ya Covid 19

Lusaka
Lusaka
Hakuna seneta atakayekubaliwa kwenda bungeni kwa mikutao ya kamati ya senate kuanzia wiki ijayo kama njia moja ya kuzuia usambaaji wa virusi vya corona .

Tangazo hilo linajiri siku  chache tu baada ya bunge la taifa kupunguza shughuli zake kwa hofu ya wafanyikazi na wbaunge kuambukizwa ugonjwa huo. Spika wa senate Ken Lusaka  amesema mikutano yote inayowalazimu maseneta kukutana ana kwa ana imefutiliwa mbal kwa mwezi mmoja ili kuzuia usambaaji wa virusi hivyo .

Spika  amesema hali itatathminiwa baada  ya mwezi mmoja  na kamati ya senate kuhusu uhasibu ndio inayoweza kuandaa mikutano  kila baada ya muda Fulani  inapohitajika .

Wiki jana spika wa bunge la taifa Justin Muturi alipiga marufuku mikutano yote ya kamati na kushauri dhidi ya mikutano yote ya ana kwa ana katika majengo ya bunge . Agizo hilo lilitolewa baada ya kuibuka ripoti kwamba huenda wabunge kadhaa na wafanyikazi wa bunge wameambukizwa ugonjwa wa corona .

Jumanne iliyopita  kiongozi wa wachache bungeni John Mbadi alifichua kwamba wafanyikazi 36 wa bunge wamepatikana na Covid 19