Kulingana na taarifa ya polisi , Saumu Mbuvi ambaye ni bintiye Gavana wa Nairobi Mike Sonko alishuhudia tukio hilo . wawili hao walikuwa pamoja .hizi hapa picha za taarifa aliondikisha Saumu .
Saumu amesema kabla ya shambulizi hilo walikuwa wakitazama fainali ya Uefa katika mkahawa wa Memphis Lounge katika mtaa wa kasarani .
Amesema wakati mchuano huo ulipotamatika ndipo alipoviziwa na mwanaume mmoja aliyeanza kumshambulia .
Ilikuwa ni wakati huo ambapo seneta Anwar aiingilia kati ili kumwokoa alipopiga kamsa . wavamizi wengine kisha walijitokeza na kuanza kumshambulia Seneta huyo na kisha kumwangusha . saumu wanasema wanaume hao kisha walianza kumwomba msamaha seneta Anwar kabla ya kutoroka .
Wakielekea kwenye gari ,walikutana tena na genge na wanaume tisa waliokuwa wamejihami kwa rungu ambao walianza tena kumshambulia seneta huyo . Saumu alipata majeraha ya mkoni alipojaribu kumkinga seneta Anwar.