Serikali yajitenga na mbunge wa Starehe, Jaguar

Serikali inasema matumizi mabaya ya Jaguar ya uhuru wa hotuba kuwafukuza jumuiya za kigeni na kuwahamasisha wanajumuiya wa eneo hilo, inadhoofisha utamaduni wa kukaribisha ambao Kenya unajulikana

Katibu wa baraza la mawaziri, Monica Juma asema kuwa lugha ya fujo na yenye hasira huenda kinyume na tabia za Kenya za kukaribisha jumuiya za kigeni na pia Katiba ya Jamhuri yetu.

Serikali imejitenga kutokana na maneneo yaliosemwa na mbunge wa Starehe, Charles Kanyi anayejulikana kwa jina lake la utani kama Jaguar.

Jaguar alitekwa kwa video ambayo sasa imeenea mtandaoni, akiwaambia wageni wa nchi za kigeni wanaofanya biashara eneo la nairobi, wazifunge na warudi nchi zao la sivyo, wataondolewa kwa nguvu.

Jaguar anahitajika kuwenda mwenyewa kwa kituo cha polisi cha Bunge.

Mbunge, aliyefungwa na wafuasi wake, alikuwa ametishia kuivamia majengo ya wageni, akiwashawishi na kuwapeleka kwenye uwanja wa ndege ambapo Idara ya Mambo ya Ndani na Uhamiaji watawafukuza.

Lakini katibu wa kudumu Macharia Kamau alisema Kenya ina majuto kwa kiasi kikubwa kwa lugha iliyotumika yenye maneno kuchochea umma yaliyotolewa na mbunge huyo..

Alisema lugha hiyo yenye fujo na yenye hasira inaenda kinyume na tabia za Kenya za kukaribisha wageni, na pia inaenda kinyume na Katiba ya Jamhuri yetu.

Serikali ya Kenya inataka kujitenga yenyewe kutoka kwa Mheshimiwa Jaguar na maneno aliyosema.

Macharia Kamau aliwathibitishia wageni wanaofanya kazi na kuishi Kenya kuwa wako salama na nchi ya Kenya itaendelea kushugulikia usalama wao.

Monica Juma aliwasihi nchi zingine ziwakaribishe wakenya na moyo mkunjufu kama walivyofanya hapo awali.