Magoha amesema kalenda ya mwaka huu ya elimu imefutiliwa mbali kwa sababu ya janga la virusi vya corona. Amesema wanafunzi wote watasalia katika madarasa waliomo mwaka wa 2021.
" Kwa ushauriano na wizara ya afya tumekubaliana kwamba shule zifunguliwe endapo visa vya covid-19 vitapungua kwa siku 14 mfululizo. Kuwatenga wanafunzi ndio jambo muhimu la kuzuia usalama wa wanafunzi wote," amesema Magoha .
" Usafiri wa wanafunzi kutoka kaunti moja hadi nyingine utasababisha changamoto kubwa kwani kuna hatari ya maambukizi ya juu.Tunafurahia kuwaarifu wakenya kwamba rais amekubali mapendekezo hayo".
Amesema vyuo vikuu vitafunguliwa tu endapo vitaafikia mahitaji yaliyotolewa na wizara ya afya pamoja na ile ya elimu.
Taasisi zote zitafanyiwa ukaguzi ili kuamua iwapo zinafaa kufunguliwa baada ya kutimiza masharti yote.
Katibu mkuu wa KNUT Wilson Sossion amesema walihusishwa katika mchakato mzima wa kuyatoa maamuzi hayo na wanaunga mkono kila hatua iliyochukuliwa na waziri Magoha .
Mhariri: Davis Ojiambo