Shule zimegeuka kuwa mahame-Walimu wakuu wasema

shule
shule
Muungano wa wakuu wa shule za sekondari umeonya kwamba shule zilizofungw ana zisizo na pesa hazitaweza kutumika tena wakati masomo yatakaporejelewa .

Muungano hu umesema  hatua ya serikali kukosa kutoa pesa  kwa shule hizo  umezilazimu shule nyingi kuwatuma nyumbani wafanyikazi wake ambao wangesaidia katika kuhakikisha kwamba  shule hizo hazigeuki kuwa mbuga  kwani nyingi zina matatizo ya nyasi kumea na hata watu kuanza kuzitumia shule kama malisho ya mifugo .

Shule kadhaa zimelazimika kuuza mifugo yao kwa sababu ya kutoweza kuwalipa wafanyikazi wa kitunza na huko Nakuru shule nyingi zimetanagaza kwamba zinauza ngombe na nguruwe  baadaya kukosa pesa za kuwalipa wafanyikazi wake .

Kampuni za ulinzi ambazo pia zimekuwa zikitoa huduma katika shule hizo  zimeanza kujiondoa kwa kutolipwa  hatua inayohatarisha mali ya thamani ya mamilioni ya pesa katika taasisi hizo .

Baadhi  ya shule zimevamiwa na vifaa vya thamani kubwa kuibwa .

Mwenyekiti wa muungano huo katika kaunti ya Nakuru    Fredrick Mbuthia  amesema changamoto zinazokabili shule hizo zinazidi kuongezeka kila uchao .