Haijabainika wazi iwapo visa hivyo vinatokana na virusi hivyo.
Nigeria kufikia sasa limethibitisha visa vya maambukizi 5,000 huku watu 164 wakiwa wamefariki.
Mkuu wa Yobe Muhammad Lawan Gana ameliambia shirika la BBC kuwa baada ya utafiti kufanyika na bainika kuwa asilimia kubwa ya watu waliofariki ni wazee huku magonjwa kama kisukari yakiwa yanaendelea kuripotiwa.
Ameongeza kuwa baadhi ya watu hao wanaofariki walikuwa wameonyesha dalili za virusi vya corona.
Tumekuwepo na taarifa kuwa asilimia kubwa ya vifo kutoka jimbo hilo la Yobe imekuwa ikifichwa swala ambalo limewapa wakaazi hofu.
Hatua ya kupima idadi ndogo ya watu katika taifa la Nigeria kubaini ni wangapi walioambukizwa virusi hivyo imetia hofu mashirika hayo yakisema huenda asilimia kubwa ya watu wanaishi na virusi hivyo