Nyota huyo hata hivyo pia amegonga vichwa vya habari kwa msururu wa vidosho ambao amehusiana nao na kisha kuwaacha hoi kila anapopata mpenzi mwingine. Diamond sio mgeni kwa sakata na amepata umaarufu sana wa kuweza kukana madai ya kuwa na uhusiano wa kimapenzi na wanawake kadhaa nchini Tanzania.
Baada ya kumuacha mpenziwe Tanasha Donna pekee yake katika hafla yake hapa Nairobi na kurejea Tanzania, wengi walishangaa ni kipi kilichomfanya Simba kurejea TZ na kumuacha Tanasha pekee yake. Umeibuka sasa uvumi kwamba huenda Mondi alirejea Tanzania ili kuwa na wakati na Hamisa Mobetto ambaye waliwahi kuripotiwa kuwa na uhusiano wa kimapenzi naye .
Hawa hapa ni baadhi tu ya wanawake wanaojulikana kuwahi kuwa na uhusiano na Diamond ingawa amekuwa akikana kuhusika katika mahusiano yoyote na baadhi yao.
Tanasha Dona
Tanasha ndiye kipenzi kipya cha Diamond na kimzaha penzi lao lilinawiri wakati staa huyo alipoachana na Zari. Wengi hawakuamini kwamba kulikuwa na uhalisia katika mipango yao ya kuishi pamoja kama wapenzi au mume na mke lakini wakathibitisha kwamba wapo ndano kwa muda mrefu ujao walipopata mtoto.
Hata hivyo uhusiano wao pia upo katika hali tete kwani hivi maajuzi, Diamond alimuacha Tanasha hapa jijini katika hafla yake na kurejea Bongo. Inadaiwa alipokuwa nyumbani, Simba alionekana na Hamisa Mobetto ! Haiwezi kutabirika kwa sasa iwapo Simba amefika kikomo lakini Diamond Platinumz hawezi kutabirika kweli.