Simba kamili! Diamond Platnumz anunua gari zito la Rolls Royce

Diamond Platnumz  amejinunulia gari zito la thamani ya shilingi milioni 45

Msanii huyo wa wimbo jeje  ameonekana akiwa na   gari aina ya  Rolls Royce likiwa na nambari ya kibinafsi  kwa jina   ‘Platnumz.’

Kwa muda sasa gari hilo limekuwa katika ndoto zake akilitamani na yaonekana simba amefaulu kulipata

Wakati fulani mwaka wa 2018 alisema katika mahojino kwamba atalinunua gari hilo ‘hivi karibuni’

Nyota huyo hajaziweka p[icha za gari hilo mtandaoni  au kutoa habari hizo kwa umma lakini tayari vidudu watu katika mitandao huko TZ tayari wameliona  gari hilo

Katika akaunti zake za mitandao ya kijamii Diamond anajitambulisha kama  mwanamuziki wa  ‘Rolls Royce  kutokla Afrika mashariki ’.

Mwaka wa 2016 nyota huo alionekana katika gari la   jeupe la  Rolls Royce  lakini baadaye ikagunduliw akwamba alikuwa akifanya video ya wimbo wake

Gari kama hilo lenye gharama ya juu ni  Rolls-Royce Phantom  linalogharimu kati ya  $450,000 ( takriban  shilingi  45,000,000).

Diamond  anafahamika kwama mpenzi wa magari na wakati mwingi huyataka kama  ‘my babies’

Tazama picha