Sio Kila Mwanamke Aliyeolewa Na Mzungu Ana Mume Wa Kiafrika - Asema Nyota Ndogo

Anapoadhimisha mwaka mmoja katika ndoa, Bi Nyota Noogo amekuja na jipya.

Kama ilivyo kawaida yake mwimbaji huyu wa Watu na Viatu ameweka picha yake na mumewe katika mtandao wa Facebok, bila shaka kumshukuru maulana.

"1year alhamdulilah.tulitrend kwa njia moja ama nyengine but MUNGU ndio anajua tunapo enda.zidi kuiongoza ndoa hii.hakuna ku edit".

Kumbuka kwamba wakati wa harusi yake wengi walikashifu vipodozi vyake lakini mwenye anakwambia la msingi ni kwamba ameolewa.

Katika  mazungumzo yetu naye Nyota anasema, ''ukiona nimeweka picha na mume wangu ni kwa sababu sina la kuficha".

Anadai kuna wanawake walioolewa na wazungu kama wengi wanavyowaita lakini kichini chini wana waume zao wa kiafrika hivyo kwao ni vigumu kuweka picha za waume zao kwa sababu wanahofia kupatikana.