Sorry:Gazeti la NY Times  laomba radhi kuhusu tangaza tata la kazi Nairobi.

New york Times hq (1)
New york Times hq (1)
Gazeti la marekani The New York Times  limetetea vikali tangazo lake la mkuu mpya wa afisi yake hapa Nairobi  lakini   afisa mkuu katika gazeti hilo amekiri   kwa kosa la kufanya mkato katika kutayarisha tangazo hilo ambalo wengi hasa wanaotumia mitandao ya kijamii hawajalipokea vizuri . Maelezo katika tangazo hilo yalionekana kutoa picha dhalilishi ya afrika na inayoonekana kutilia mkazo dhana potovu  ambayo wageni huchukulia bara afrika na watu wake .

Mhariri mkuu wa kimataifa  Michael Slackman akijibu video  yenye ucheshi kukejeli tangazo la kazi hiyo  amejitetea akisema wamejitolea kuchapisha  na kuueleza ulimwengu kuhusu matukio ya  bara afrika lakini sio kwa ajili ya dhana  dhalilishi na udunishaji  wa maisha ,mfumo wa uongozi  na uendeshaji wa masuala ya waafrika . Wiki jana  New York Times  ilichapisha tangazo ikisema inamtafuta mwandishi anayefaa kuwa mwepesi wa ‘kurukia ‘ taarifa  ili kutangaza kuhusu mizozo , na pia kuvutiwa na taarifa za upekuzi .

Tangazo hilo  halikuwapendeza watumizi wa mitandao ya kijamii

 “Our Nairobi bureau chief has a tremendous opportunity to dive into news and enterprise across a wide range of countries, from the deserts of Sudan and the pirate seas of the Horn of Africa, down through the forests of Congo and the shores of Tanzania,”  Ilisoma sehemu ya tangazo hilo kwa lugha ya kiingereza  .

Lakini Slackman  ambaye hapo awali amewahi kufanya kazi  Cairo, Berlin, Moscow, Albany na  Melville  amekiri kuhusika na uandishi wa tangazo hilo  na amesema anajutia kwa kutochukua muda  ufaao kutayarisha maelezo  yanayokubali ya akina ya waandishi na  kazi waliofaa kuifanya badala ya kutumia maneno yaliotafsiriwa kulidunisha bara la afrika .