Sponsor hataki nipate boyfriend na hanitoshelezi kitandani

Kila siku katika kipindi cha Bustani la Massawe, ambacho huletwa kwako na mtangazaji Massawe Japanni, mijadala kadha wa kadha huchipuka.

Mijadala hii huwa ya ku elimisha, kushangaza na pia ya kuvunja moyo kwani zaidi ya mamilioni ya wakenya huwa tayari kusimulia yanayowakumba.

Hivi majuzi Massawe aliwaomba waskizaji wake wachangie kuhusu maisha ya kuwa kwa uhusiano na sponsor.

Mwanadada mmoja alilalamika kuwa yeye yuko kwa uhusiano na sponsor ambaye anamlisha, anampa fedha na kila kitu anachotamani lakini amelegea sehemu ya kitandani.

Cha kushangaza ni kuwa mwanadada huyo ana miaka 23, huku sponsor wake akiwa na miaka 52.

Alilalamika kuwa anahitaji mwanaume mwenye nguvu ya kijana wa mika 24.

Alipoulizwa mbona asitafute kijana wa umri wake alisema kuwa ameshindwa kumuacha yule mume kwani anampa fedha vilivyo.

Soma usimulizi wake.

Mimi niko naye Massawe, lakini sasa shida ya sponsor hakuridhishi, jamaa akikuhitaji atakuhitaji lakini ikifika mambo ya Mombasa raha mjamaa anashindwa na hataki u chat na mtu anaweza kazi.

Nimeshindwa sasa nitafanya vipi? Ana pesa kwani anatoboka vizuri, ana miaka 52 nami nina 23.