- Sonko Alikuwa ameratibu mkutano na Jeff Koinange
- Rafikiye Maribe aiambia mahakama kwamba walikuwa kituoni hadi Sonko alipomaliza mahojiano yaje na wakaondoka saa tano unusu usiku pamoja na Maribe hadi eneo la burudani la Club 40/40, Westlands. Walisalia huko hadi saa Kumi alfajiri .
Mtangazjai wa zamani wa habari Jacque Maribe alikuwa na gavana wa Nairobi Mike Sonko siku ambayo Monica Kimani aliuawa ,mahakama ilielezwa siku ya jumatano . Mmoja wa mashahidi katika kesi ya mauaji ya Monica ,rafiki ya Maribe Chelagat Ruto ameiambia korti kwamba Maribe alikuwa pamoja na Sonko usiku wa mauaji hayo .Ruto alisema kwamba septemba tarehe 19 mwaka wa 2018 alienda eneo la Road House Grill na rafiki yake mmoja mwendo wa saa kumi na mbili unusu jioni na walikutana na Joseph Irungu al maarufu Jowie akiwa na rafiki yake .Walipata chakula cha mchana . Maribe na mpenziwe wa zamani Jowie wameshtakiwa kwa mauaji ya Monica Kimani ,shtaka wanalokanusha .Ruto anasema Jowie alikuwa na kaptula ya rangi ya brown yenye mifuko ya pembeni na kofia ya rangi ya maroon na Tshirt ya rangi nyeupe . Waliitisha nyama choma na viazi na kula pamoja wakipiga gumzo . Chelegat amesema Jowie alikuwa akibugia kileo cha Vodka na rafiki yake ilhali naye alikunywa maji . Amesema alikuwa huko kumtayarisha Sonko kwa mahojiano yaliopangwa katika kipindi cha JKL usiku huo. Mwendo wa saa mbili unusu usiku , Jowie na rafiki yake wa kiume waliondoka sehemu hiyo na akamtumia rafiki yake Juliet pesa kupitia huduma ya Mpesa kulipia bili .Ruto alisema alikutana na Maribe mwaka wa 2017 wakati wa kampeini za uchaguzi mkuu ambapo alikuwa katika kundi la kampeini za seneta Johnson Sakaja .
Ameiambia mahakama kwamba baadaye walikuuza urafiki na Maribe alimtambulisha kwa Jowie .Mahakama iliambiwa kwamba mwendo wa saa tatu usiku aliondoka Road House Grill na kuliegesha gari lake jeupe la Range rover katika eneo la Q lounge linalokaribiana na afisi za Royal Media services . Waliingia katika jumba hilo la habari na kumpata Sonko ,wakamtayarisha kwa mahojiano na walipokuwa katika ukumbi wa kungojea watu ,walikutana na Maribe aliyekuwa akifanya kazi .Ruto ameiambia magakama kwamba walikuwa kituoni hapo hadi Sonko alipomaliza mahojiano yake na wakaondoka saa tano unusu usiku wakiwa na Maribe kwenda 40/40 mtaani Westlands.Ruto amesema walikuwa Club 40/40 pamoja na Sonko hadi mwendo wa saa saba usiku wakati Jowie alipojiunga nao .Walisalia huko hadi mwendo wa saa kumi alfajiri .
Jowie alielkea katika meza waliokuwa na kuwasalimu kabla ya kurejea katika meza ndogo ya watu wawili na kuagiza Tusker Lite. Ameiambia mahakama kwamba aliondoka kilabuni humo pamoja na Juliet katika gari lake ilhali Maribe aliondokana katika gari lake pamoja na Jowie . Alisema siku chache baadaye alipata habari za kuuawa kwa mwanamke mmoja katika nyumba yake mtaani Kilimani . Amesema alishangazwa kwamba Jowie na Maribe ambao hawakuwa na tofauti zozote naye walihusishwa na mauaji hayo . Msimamizi na mfanyikazi wa bustani za nyumba za Lamuria Apartments pia walitoa ushahidi wao . Msimamizi huyo Reagan Buluku na mfanyikazi wa shambani Stephen Wanjohi wote walisimulia jinsi walivyoupata mwili wa Monica .
Mahakama ilifahamishwa kwamba walikuwa wakitoka kwa chakula cha mchana septemba tarehe 20 na kukutana na kakake Monica George pamoja na mchumbake .George anaripotiwa kumtaka Buluku amsaidie aingie katika nyumba ya dadake kwa sababu hakuwa akichukua simu na baadaye simu hiyo ikazimwa .Buluku alisema kwamba walipofika katika nyumba ya Monica ,runinga ilikuwa imewashwa na maji yalikuwa yakisikika yakitiririka kutoka mferejini .Buluku kasha alimwambia Wanjohi kuleta ngazi ili waweze kuifikia ghorofa ya tatu ili waweze kuifikia nyumba ya Monica kupitia Jikoni . Wanjohi aliitumia ngazi hiyo na kuingia chumbani mwa Monica kupitia dirishani .Anasema hakuweza kumwona Monica popote na pia alikuwa akiutafuta ufunguo ili aweze kuufungua mlango ili mradi awawezesha wengine kuingia katika nyumba ya Monica . Anasema alielekea katika chumba cha kulala lakini hakumwona yeyote licha ya kutazama sehemu nyingine za nyumba nzima .Baadaye aliamua kwenda kuangalia bafuni . Aliuona mwili wa Monica ukiwa katika tabu ya kuogea .maji ya mfereji yalikuwa bado yanamwagika katika tabu hiyo .
Kulingana na msimamizi na mfanyikazi wa shambani ,mikono yake yote na miguu ilikuwa imefungwa na koo lake kukatwa ,na kuongeza kwamba kuliwa na damu katika shingo lake .Wanjohi alipiga kamsa na kuwaambia waliokuwa nje wauvunje mlango kwa sababu mambo hayakuwa mazuri mume ndani .Buluku alipata kifaa cha kutumia na wakavunja mlango kasha wakaingia katika nyumba ya Monica .