Je ni nini kinachoendelea kati ya King Kiba na Diamond Platnumz?
Vita hivi vilianza na Ali Kiba kumuanika Diamond na kumwambia awache tabia za kitoto, haswa tabia za watoto wa darasa la pili.
''USINILETEE MAMBO YA DARASA LA PILI UNANIIIBIA PENSELI ALAFU UNANISAIDIA KUTAFUTA .(UNIKOME). ''
Zaidi ya hayo, Ali Kiba alisema,
''MWANAUME HUWA ANAONGEAGA MARA MOJA TU SASA UKITAKA NIKUWEKE UCHI WATU WAJUE UNAYONIFANYIA HATA KWENYE HILO TAMASHA HATOKUJA MTU SASA TUISHIE HAPO NAKUTAKIA TAMASHA NJEMA @DIAMONDPLATNUMZ''
Baada ya ujumbe huo wa King Kiba, Diamond alijibu ujumbe wake na kusema kuwa King Kiba ana mawazo mengi na ndio maana anazungumza akiwa na machungu sana.
''MMESIKIA ANAELILIA PENSELI? STRESS HIZI'' Diamond alisema.
Haijulikani kama wanamziki hawa wanarushiana maneno makali kwa sababu hawasikizani ama ni matani tu kwani urafiki wao huwa haueleweki vyema.