SUTI ZA MWILI WA MOI :Mwili wa Mzee wavalishwa suti tofauti kila siku unapotazamwa .

Rais Uhuu Kenyatta na mkewe Margaret wautazama mwili wa Mzee Moi
Rais Uhuu Kenyatta na mkewe Margaret wautazama mwili wa Mzee Moi
Mwili wa marehemu Mzee Daniel Moi  ulivalishwa suti tofauti kila siku ambayo ulipelekwa bungeni kutazamwa na wananchi .

  Siku ya jumatatu ambayo ndio ya mwisho mwili huo kuwekwa katika majengo ya bunge ili kutazamwa na umma , mwili wa Moi ulivalishwa  suti ya rangi ya kijivu (grey) ,viatu vya  rangi ya  kahawia(brown) ,shati jeupe na  tai yenye vistari vya  manjano . Kirungu kidogo cha mzee Moi al maarufu fimbo ya nyayo  kiliwekwa katika mkono wake wa kulia kinyume na siku mbili za awali ambapo kiliwekwa kando yake . Siku ya kwanza ya kuutazama mwili huo jumaosi  ,ulivalishwa  suti ya  rangi ya kijivu  shati jeupe na viatu vya  rangi ya kahawia  na tai yenye maua . Siku ya jumapili iliyokuwa ya pili kwa mwili wake kutazamwa na umma ,alivalishwa  suti nyeusi ,shati jeupe ,tai ya rangi nyekundu na  viatu vyeusi .

 

 Viongozi ambao tayari wameuona mwili wa Mzee Moi ni pamoja na rais Uhuru Kenyatta ,naibu wake William Ruto ,rais mstaafu  Mwai Kibaki ,mabalozi ,wabunge  na maseneta,magavana na viongozi wa kidini .

Rais huyo wa zamani atapewa taadhima zote za kijeshi   wakati wa maazishi yake ikiwemo saluti ya milio 19 ya risasi . Siku ya jumanne misa ya madhehebu mbali mbali itafanyika katika uwanja wa Nyayo Nairobi . Moi atazikwa nyumbani kwake Kabarak siku ya jumatano .