Awali ungesimuliwa kwamba kitu kama hicho kinafanyika basi ungesema labda katika filamu lakini masimulizi ya wahusika yamethibitsha kwamba kweli tabia hiyo inafanyika hapa kenya . Elimily* na Karis ambao wamejiunga kundi hilo la siri wanasema walipatana na pendekezo hilo kupitia rafiki yao mmoja ambaye aliwaambia jinsi mtindi huo hutekelezwa na baada ya kuwashawishi kuhusu umuhimu wa kufanya hivyo ili kuboresha ndoa yao ,basi walikubali na wakawekwa katika kundi moja la whatsapp ambalo lilikuwa na wanachama wengine wanaofanya hivyo na waliojipa jina ‘Nairobi Swingers’.
Mwanzoni walipatwa na hofu kuhusu watakavyojiingiza katika mtindo kama ule kwamba Emily angelala na mwanamme mwingine kisha Karis afanye mapenzi na mwanamke mwingine .Walikaribishwa katika kundi hilo katika mkutano uliofanyika kwenye mtaa moja wa kifahari kisha wakatambulishwa kwa wanachama wengine . Pale ,zililetwa picha za wanawake wote ambao wapo katika lile kundi na Karis alitakiwa kumchagua mmoja. Aliambia wkamba mume wake alikuwepo pale pia lakini hilo halikufaa kumpa wasi wasi .Wakati unapomchagua mwanamke wa mwenzio ,basi huyo ndiye unayefaa kulala naye kwa usiku mmoja na mkeo pia atachaguliwa na mwanamume mwingine . Kulikuwa na masharti kwamba huwezi kufanya mapenzi na mke wa mwenzio bila kinga na wote walisaini stakabadhi ya kueleza hilo .
Emily naye aliletewa picha za wanaume ambapo alifaa kumchagua mmoja wa kulala naye usiku mmoja .mke wake alikuwepo katika kundi hilo na baada ya kuchagua sasa walijumuika pamoja huku kila mmoja sasa akijua ni yupi aliyemchagua mke wake au mume wake .Ilipangwa safari ya kwenda karamu ya kujivinjari Naivasha ambako Elimy na Karis walikaribishwa kwa kundi la swingers kwa kulala na watu wan je .Tangia hapo wamezoea na sasa ni wanachama wa kundi hilo ambapo kila wanapopiga safari ,wao huchaguana upya kila mmoja akiamua yuataka kulala na mke au mume wa nani .Majabu!a