Taarifa ya Habari Toleo la saa Kumi 16/10/2019

RADIO JAMBO MIC
RADIO JAMBO MIC
WASHUKIWA tisa  wakiwemo maafisa sita wa polisi waliokamatwa kuhusiana na wizi wa shilingi milioni 6  kutoka kwa wafanyibiashara wawili mtaani eastleigh  wameachiliwa kwa bondi ya shilingi milioni 1 kila mmoja .washukiwa hao  ni pamoja na raia wawili na  raia mmoja wa cameroun  walionaswa katika kamera ya cctv wakitekeleza  uhalifu huo octoba tarehe nne .

Vijana wametahadharishwa dhidi ya kukubali kugawanya na wanasiasa .rais Uhuru Kenyatta amesema  vijana wanafaa kuzingatia ustawi wao na wa nchi bila kujali makabila yao kwa lengo la kuhakikisha kwamba mustakabali wao ni mzuri .

Waziri wa elimu  George magoha amesema  marekebisho  katika  vyuo vikuu  lazima yatekelezwe  kwani  haisadii kuwa na vyuo vikuu vingi vinavyotoa ubora wa chini wa elimu . magoha amesema heri kuwa na  vyuo vikuu vichache vinavytoa elimu bora

Gavana wa  Taita Taveta granton samboja  atajua hatma yake katika kipindi cha siku 10 zijazo wakati  kamati ya senate ya wanachama 11 iliyoundwa kuchunguza kufurushwa kwake afisini  itakapotoa ripoti  yake . kamati hiyo itaangazia lalama zilizoibuliwa dhidi ya samboja  ikiwemo kukosa kutoa mwongozo kuhusu utayarishaji wa bajeti.

Kiongozi wa Thirdway Alliance Ekuru Aukot  amelaumu ufisadi , ubarakala wa kisiasa na vitisho kama sababu zinazowafanya waakilishi wa kaunti kuukata mswada wake wa punguza mizigo . Aukot ameashiria kwamba huenda akaelekea mahakamani ili kupinga sababu zinazotolewa na mabunge ya kaunti kuukata  mswada huo .