TAKRIBAN asilimia 20 ya wapiga kura wameshapiga kura katika uchaguzi mdogo wa wadi ya ganda huko kilifi .afisa msimamizi wa uchaguzi Juma Musa amesema wengi wamezuiawa kufika vituoni kupiga kura kwa ajili ya mvua iliyoanza kunyesha leo asubuhi .
Maseneta wamezuiwa kujadili au kuendelea na mchakato wa kushughulikia hoja ya waakilishi wa bunge la taita taveta kumwondoa afisini gavana granton samboja hadi kesi ambayo gavana huyo amewasilisha kortini isikizwe na kuamuliwa . samboja amesema maseneta walipuuza agizo la awali la mahakama na kuunda jopo la kuchunguza madai yaliyotolewa dhidi yake .
Biwi la simanzi limetanda katika kijiji cha okook kaunti ndogo ya teso kusini HUKO busia baada ya mwanafunzi mmoja wa kike wa kidato cha kwanza katika shule ya upili ya mseto ya st .Mark machakus kuuawa baada ya kupigwa na radi .jenipher amoit anasema kuwa mwanawe lydia emwatok alipigwa na radi nyumbani kwao saa moja jioni alipokuwa akianika sare zake za shule.
Mbunge wa malindi Aisha Jumwa na mlinzi wake wameagizwa kufika mbele ya DCI jumanne wiki ijayo ili kuwasaidia katika uchunguzi kuhusiana na rabsha zilizotokea katika wadi ya ganda na kupelekeea kuuawa kwa mtu mmoja . wameachiliwa kwa dhamana kwa ajili ya ukosefu wa ushahidi .
Baadhi ya barabara mjini Mombasa hazipitiki kwa ajili ya mvua kubwa inayoshuhudiwa katika eneo hilo .idara ya utabiri wa hali ya anga imesema kiasi cha mvua kitazidi huko pwani hadi jumapili .
Wanafunzi wawili waliopotea kutoka shule ya wavulana ya utumishi huko gilgil wamepatikana wakiishi hapa Nairobi na binamu zao baada ya kutafutwa kwa wiki mbili . wawili hao ambao ni watahiniwa KCSE walitoweka kutoka shuleni humo katika hali ya kutatanisha .