NI MATAJIRI KUPINDUKIA! Wanaume 22 matajiri duniani wana mali inayotoshana na wanawake milioni 325 Afrika

Watu matajiri zaidi duniani .Wana jumla ya mali yenye thamani ya Dola Bilioni 426.
Watu matajiri zaidi duniani .Wana jumla ya mali yenye thamani ya Dola Bilioni 426.
Wanaume 22 matajiri zaidi ulimwenguni wana jumla ya mali inayotoshana na na mali ya wanawake  milioni 325 barani  Afrika ,kulingana na shirika la  Oxfam International. Ripoti moja ya shirika hilo imeonyesha kwamba watu 2,153  kote duniani  wanathibiti pesa na mali  zaidi ya watu bilioni 4.6 kote duniani  ingawaje hawafanyi lolote kubadilisha ufukura wa jamii .

Ufichuzi huo kuhusu ukosefu wa usawa katika ugavi wa utajiri umo katika ripoti ya kurasa 64 ya Oxfam  iliyotolewa siku ya jumatatu  wakati wa kongamano la uchumi wa dunia WEF huko  Davos, Switzerland.  Oxfam ,yenye makao yake jijini Nairobi imesema ukosefu huu wa usawa umesababishwa na ugavi wa kibaguzi wa utajiri unaoegemea jinsia moja  na unaowapa kipau mbele wachache walio navyo.  Shirika hilo limesema serikali nyingi ulimwenguni hazijachukua hatua za kurekebisha tatizo hilo

“ wanawake na wasichana ni miongoni mwa wanaokosa kunufaika ipasavyo na mfumo wa sasa wa uchumi wa ulimwengu . wanatumia mabilioni ya saa kupika ,kusafisha na kuwatunza watoto na wazee’ amesema   afisa mkuu mtendaji wa OXFAM  India  Amitabh Behar. Ripoti hiyo imesema wanawake na wasichana  walitumia saa bilioni 12.5 kufanya kazi wasizolipwa  kila siku  ambazo zilichangia  ($10.8 trillion) kila mwaka katika uchumi wa dunia.

“ Wanawake wanafanya zaidi ya thuluthi nne ya kazi yote ya utunzi isio na malipo .Wao hulazimika  kupunguza saa zao za kufanya kazi  au kuacha kazi kabisa ili kushughulikia kazi za utunzi’.

“ Kazi kama vile za walimu wa shule za chekechea ,wafanyikazi wa nyumbani na wasaidizi  huwa na mlipo ya chini sana na manufaa  adimu  kando na kwamba zinahitaji muda mwingi wa kuzitekeleza  na zinasababisha uchovu wa kimwili’ Ripoti hiyo imeongeza .