Watatu hao ni katibu msimamizi wa wizara ya ardhi Gideon Mung’aro, mbunge wa Laikipia kaskazini Sarah Korere na mfanyibiashara wa pwani Suleiman Shahbal. Wote walikuwa katika afisi za Raila za Capital Hill ili kutangaza misimamo yao kujiunga na mrengo wa rais na bwana Odiga huku wakijitenga na kundi la tanga tanga. Wa kwanza kuvuka laini na kujiunga na upande wa pili ni mwakilishi wa akina mama wa Laikipia Catherine Waruguru. Korere wakati mmoja alikuwa mtetezi sugu wa DP Ruto na kauli zake za pingamizi dhidi ya sera za rais Kenyatta na azama ya kisiasa ya Bwana Odinga zinafahamika na wengi. Pia amekuwa mksoaji mkubwa wa mwafaka wa handshake kati ya rais Kenyatta na Odinga.
Alikuwa miongoni mwa wajumbe wa Jubilee waliolengwa na shoka la kutimuliwa kutoka kamati za bunge lakini sasa amejitokeza na kutangaza kwamba anaunga mkono mwafaka wa handshake na BBI. Alikuwa ameandamana na seneta wa Narok Ledama ole Kina alipotangaza kujiunga na mrengo wa Uhur-Raila Kutoka kundi la tanga tanga.
“ Nimempokea mbunge wa Laikipia North Sarah Korere ambaye ameunga mkono jitihada za kuliunganisha taifa’ Raila aliandika katika twitter muda mfupi baada ya kukutana na mbunge huyo.
Tangu chama cha Jubilee kiwafurushe viongozi wa seneti na bunge waliokuwa katika mrengo wa Ruto kutoka nafasi za uongozi, baadhi ya wabunge kutoka mrengo wake wamekuwa wakizingatia kubadilisha misimamo kisiasa ili waweze kuepushwa na shoka la kuonyeshwa mlango. Gazeti la The Star limeripoti kugundua kwamba wabunge wengi wanaomuunga mkono Ruto ambao wanalengwa kuondolewa katika kamati za bunge wanapanga kukutana na Raila wiki zijazo .
Ruto Ruto amesalia kimya tangu shoka kuwakuta washirika wake Kithure Kindiki wa Tharaka Nithi, Kipchumba Murkomen wa Elgeyo Marakwet, Susan Kihika wa Nakuru, Benjamin Washiali wa Mumias mashariki na Cecily Mbarire(Mteule). Raila pia amekutana na mwanasiasa wa pwani CAS Mung'aro na Shahbal ili kujadili masuala mbalimbali yanayohusu ‘maendeleo ya eneo la pwani’.