Tangatanga yasalimu amri: Wabunge kuhudhuria mikutano ya BBI

Tanga tanga
Tanga tanga
Wabunge wanaomwunga mkono naibu wa rais William Ruto sasa wametangaza kwamba watahudhuria mikutano ya hadhara ya kuipigia debe ripoti ya BBI .

Kiongozi wa walio wengi katika senate Kipchumba Murkomen amewashtumu viongozi walio katika mrengo wa rais kenyatta na kiongozi wa ODM Raila odinga kwa kuwa na  kamati ya siri yenye ripoti tofauti ya BBI ambayo wanalenga kuipendekeza kwa wakenya .

" Tumehofishwa na ripoti kwamba kuna  kamati ya siri yenye ripoti tofauti ya  BBI .Tunaitisha uwazi katika mchakato mzima wa kutekeleza mapendekezo ya ripoti ya BBI’ amesema Seneta Murkomen. Murkomen  alikuwa akizungumza pamoja na wenzake  Susan Kihika (Nakuru), Moses Kuria (mbunge wa Gatundu kusini ) Alice Wahome (mbunge wa Kandara)  na wajumbe wengine .

" Badala ya kuzungumzia masuala husika ,mikutano ya BBI ya kisii na Kakamega  ilibadilishwa na kuwa ya kumcafulia jina mtu mmoja’ aliongeza Murkomen . " Tunapinga  kutumiwa kwa fedha za umma kuendesha mikutano hiyo ya hadhara  endapo matumizi ya pesa hizo hayataidhinishwa na bunge au mabunge ya kaunti’

Wanasiasa wameshtumiwa kwa kuliteka nyara  suala zima la utekelezaji wa BBI  huku wananchi wakinyimwa fursa ya kutoa maoni yao  kuihusu ripoti hiyo . wakati wa mikutano ya Kisii na Kakamega ,wengi waliopewa fursa za kuzungumza ni magavana na wabunge .

wanachama wa vuguvugu la mashirika ya kiraia wamesema wanahofishwa na jinsi mchakato mzima wa mikutao ya BBI unavyoendeshwa kwa sababu wananchi wameachwa nje .