Waituti, mkewe Susan wangari na wengine wanane wanakabiliwa na mashtaka ya ufisadi kuhusiana na kandarasi zenye thamani ya shilingi milioni 580 ambazozilitolewa kwa kampuni zinazodaiwa kutoa hongo . Waakilishi wa kaunti ya kiambu walimwondoa waittu afisini mwezi uliopita na sasa senate inangoja kufanya kikao siku ya jumanne ili kuamua hatma yake .
Tangu mwaka wa 2013 senate imeidhinisha tu kuondolewa maamlakani kwa gavana mmoja . Duru zaarifu kwamba maseneta wanaomwunga mkono rais Kenyatta wanashirikiana na maafisa wenye ushawishi mkubwa katika ikulu ,ili kuhakikisha kwamba uamuzi wa walkilishi wa kaunti ya Kiambu wa kumfurusha Waititu afisini unatekelezwa . Waititu mwenyewe amepinga vikali kuondolewa kwake akidai kwamba bunge la kaunti halikuwa na idadi inayohitajika ya waakilishi wa kaunti kuufanya uamuzi huo .