Tanzia: Mbunge wa zamani Hezron Manduku afariki

Manduku
Manduku
Aliyekuwa mbunge wa  Nyaribari Masaba  Hezron Manduku  ameaga dunia katika Nairobi Hospital  alikokuwa amelzwa . Mbunge huyo wa zamani amefariki akiwa na umri wa miaka 79 amethibitisha mwanawe  Dr Robert Manduku.Dr Manduku  amekuwa akiugua  ugonjwa usioweza kutibiwa kwa muda mrefu . Viongozi kadhaa wametuma risalam za rambi rambi akiwemo mbunge wa sasa wa Nyaribari Masaba  Ezekiel Machogu .

Mbunge wa Nyaribari Chache  Richard Tong’i  amemtaja marehemu Manduku kama kiongozi aliyekuwa na maono na aliyejizatiti kuboresha  hali ya  maisha ya wananchi . Marehemu   Dr Manduku  alichaguliwa kwa mara ya kwanza bungeni mwaka wa 1992 kwa tiketi ya chama cha KANU   lakini baadaye akapoteza kiti hicho kwa seneta wa Kisii Sam Ongeri mwaka wa 1997. Baadaye alikihama chama cha KANU na kujiunga na  Ford People  alipokishinda kiti hicho mwaka wa 2002.

Dr Manduku  na  Prof Ongeri walihudumu kama wabunge wa Nyaribari Masaba kwa zaidi ya miongo miwili huku kila mmoja akikiri kwamba ni mwingine tu angeyeweza kumshinda  mwenzake kutoka uongozi . Baadaye pia alihudumu kama waziri msaidizi wa  Mashauri ya kigeni  kati ya mwaka wa 1993 na 1997 .