Bunge la kaunti ya Nakuru limepata pigo baada ya kuaga dunia kwa mmojawapo ya waakilishi wake wa kaunti kupitia ajali ya barabarani kwenye barabara kuu ya Nairobi Kwenda Nakuru.
Mwakilishi wa wadi ya Lake View Karanja Mburu alifariki baada ya gari lake kupoteza mwelekeo na kugonga mti katika eneo la View Point kilomita kumi kutoka mji wa Gilgil jumapili asubuhi .
Mwakilishi huyo wa kaunti alikuwa mshirika wa karibu wa Naibu wa rais William Ruto na seneta Susan Kihika alikuwa pekee yake akielekea Nakuru kutoka Naivasha wakati ajali hiyo ilipotokea.
Saa kadhaa baada ya ajali hiyo Gavana wa Nakuru Lee Kinyanjui ,spika wa kaunti Joel Maina na waakilishi kadhaa wa kaunti walifika katika katika eneo la mkasa ili kumuomboleza Mburu .
Akithibitisha ajali hiyo OCPD wa Gilgil Emmanuel Opuru ,amesema mti huo uliogongwa ulifunika sehemu ya mbele ya gari hilo na kuwazuia madereva wengine kuuona .