Rais mstaafu Daniel Arap Moi ameaga dunia .Rais Uhuru kenyatta ametoa taarifa akitangaza kifo cha Mzee Moi ambaye ameaga dunia akiwa na umri wa miaka 95. Mwezi uliopita madaktari katika hospitali ya Nairobi walilazimika kumrejesha Moi katika mashine za kumpa usaidizi wa kupumua .Hali yake ya afya imekuwa maaya tangu oktoba mwaka jana alipolazwa hospitalini .
Wakati huo alipolazwa hospitalini ,msemaji wake Lee Njiru alisema Moi alikuwa amekwenda hospitali kwa ukaguzi wa kawaida lakini tangia hapo alilazwa hospitalini mara nne. Kundi lake la madaktari likiongozwa na Daktari David Silverstein limekuwa likimpa mkatibabu kwa matatizo yanayojirejeeza na kumfanya kusalia kitandani kwa miezi mitatu .
Hali ya afya ya Mzee Moi ilizidishwa kuwa mbaya na jeraha la goti alilopata wakati wa ajali iliyohusisha gari lake mwaka wa 2006 huko Limuru .