Mchezaji wa raga ya wachezaji saba kila upande Tony Onyango ameaga dunia . Ripoti zaarifu kwamba Onyango alianguka akiwa katika nyumba yake mtaani Ngong jana usiku na kufariki .
https://twitter.com/EricNjiiru/status/1235061468808097792
Aliichezea Kenya simbas kuanzia aprili mwaka wa 2012 kwa miaka sita kabla ya kuhamia Homebpoyz na maajuzi amekuwa akiichezea KCB . Onyango alikuwa nahodha wa timu ya raga ya shule ya Maseno mwaka wa 2009 na pia aliichezea Kenya sevens katika msimu wa mwaka wa 2014/2015 chini ya kocha Paul Treu.
https://twitter.com/ItsMoe254/status/1235074720715943936
Mashabiki wengi wa raga walituma risala zao za rambi rambi kwa familia yake baada ya kupata habari za kifo cha mchezaji huyo .