Toboa siri: Nakuta vitu za shemeji wangu

Katika kitengo cha Toboa siri ambacho huletwa kwako na watangazaji nguli, Mbusii na Lion, hivi majuzi kilishuhudia tukio la kukata na shoka.

Jamaa mmoja aliomba kutoboa siri huku akimtobolea mkewe kuwa amekuwa akishiriki ngono na dadake bila yeye kujua. Isitoshe angependa kumwambia mkewe kuwa ana mipango ya kumuoa kama mke wa pili.

Cha kushangaza, jamaa huyu alidai kuwa hajalishwi na mkewe kwani kile anaweza fanya ni kumkasirikia kisha mambo yaishe, na kama atamtenga atawasilisha kesi kwenye kitengo cha patanisho.

Soma usimulizi wake,

Hii siri ni, nina wife halafu sister yake alikuja kunitembelea na tukakaa nayeye na sasa naona ananipenda hata kuliko bibi yangu mwenyewe. Sasa ananiambia nimtafutie nyumba ili awe mke wangu wa pili, na nilishatest ile siku Gor Mahia ilicheza na Everton.

Sister in law ana miaka 25 na bibi yangu ana 28 na tumeishi pamoja kwa miaka mitatu na tukabarikiwa na mtoto mmoja.

Sasa nataka nikitoboa hiyo siri bibi yangu ajue na kabla ajue wanaJambo waniambie nifanye nini, nimchukue kama mke wa pili au aje kwani kusema ukweli nahisi kumchukua.

Mke wangu akiskia nimechukua dadake atafura tu kwani pia yeye ananipenda. Akiniacha nitaleta maneno mnisaidie tena.

Pata uhondo kamili.