Carey ambaye ni mtaalam wa kuwapodoa watu na kuwarembesha amekuwa akifanya kazi na 'macelebs' wengi nchini lakini sasa mtindo wake wa mavazi na miondoko yake mitandaoni imemfanya kujipa nafasi pia kama 'celeb'. Amekuwa akifanya uigizaji na pia ni model .
Licha ya imai yake ambayo wengi wanaitazama kuwa yenye maadili makali ya kiroho, Carey amevunja mipaka ya mafanikio yake. Katika kazi yake yupo katika kundi la walio kileleni na iwapo ulikuwa unamtafuta msanii wa 'make up' basi umepatana na fundi wa wote .
Carey pia amefahamika kwa kuendeleza miundo ya mavazi ya kisasa na picha zake katika mitandao ya kijamii zinatoa taswira ya mapenzi yake kwa fani ya fasheni. Hapa tazama msururu wa picha zake zikupe kasi ya moyo .