Inadaiwa wawili hao walitengana mwezi mmoja uliopita. Duru zinasema wawili hao walianza kupata matatizo baada ya Prude kugundua kwamba mume wake alikuwa na mahusiano ya pembeni. Inadaiwa wawili hao walikuwa wakiishi katika mtaa wa Phenom kabla ya kuihama nyumba yao .
“ Mwezi machi mambo yaligeuka na kuwa mabaya wakati raburu alipomnyaka mkewe kuondoka. Sasa anaishi kileleshwa na mwanamke mwingine."
Kidudumtu aliyetoa ufichuzi huo amekiri kwamba mkewe Raburu anaishi katika nyumba ya kukodi katika eneo la Thindigua, Kiambu
“ kilichofanyika ni kwamba waligawana vitu vya nyumbani. Baadaye Raburu akampangishia Marya Nyumba na kulipa kodi ya miezi miwili
Marya amefuta akaunti zake za mitandao ya kijamii. Wakati wa mwisho Raburu kuweka mtandaoni picha ya mkewe ilikuwa siku ya kuwaadhimisha mama duniani .
Raburu alifunga ndoa na Marya miaka miwili iliyopita ambapo ni jamaa na marafiki wa karibu ndio walioalikwa pekee. Mapema mwaka huu, wawili hao walipoteza mtoto wao ambaye bado hakuwa amezaliwa wakati Marya alipokuwa mja mzito .
Mpasho imesema ilipojaribu kuwasiliana na Raburu, hakujibu lolote juhudi zao za kuwasiliana na Marya pia zimeambulia patupu.