Akiielezea kama Tsunami, Raila alitangaza kuwa Ruto na kikosi cha TangaTanga watabumburushwa na upepo huo mkali wa kisiasa na kubwagwa katika bahari.
Soma hapa:
"Nimetazama angani na kuona mawingu yametanda,"Raila alihutubia wananchi waliojawa na furaha mtaa wa Kibera
"Ni ishara kuwa mvua itanyesha muda usio mrefu. Kuna upepo mkali unaovuma kutoka mashariki kwenda magharibi, kaskazini kwenda kusini. Utavurusha uchafu wote wa TangaTanga baharini."alisisitiza kinara wa upinzani.
TangaTanga ni kikundi kinachohusika kumpigia debe na kumuunga mkono naibu wa rais.Hali kadhalika, Kieleweke ni kikundi kinachounga mkono lengo kuu la kuunga mkono BBI na kuhakikisha ajenda kuu za Rais Kenyatta zimetimia.
Ruto ameipinga BBI huku wanaomzunguka wakisema kuwa Raila anatumia "Handshake" yake na Rais Kenyatta kusambaratisha ndoto za Ruto kuwania urais mwaka ujao wa 2022.
Soma hapa:
"Viongozi wengine waache vitisho. Hatutakupatia nafasi ya kugawanya nchi hii. BBI ikileta mapendekezo yake tutajihusisha katika mjadala.Hatutakubali Tsunami kugawanya nchi hii." Alisema Ruto.