Watoto hao wa Kibor walipoteza kesi kortini ambayo Mzee Kibor alitaka wafurushwe kutoka shamba la la ekari 1200 huko Soy ,Uasin Gishu . Watoto hao wamesema wanafahamu kwamba baba yao mwenye umri wa miaka 88 anapanga kuwafanyia vipimo vya DNA ili kujua iwapo ni watoto wake kabla ya kuanza kuwagawia mali
Mmoja wao Ezekiel Kipng’etich, amesema watakubali tu kufantyiwa vipimo hivyo katika taasisi ya serikali ambako matokeo hayatabadilishwa kwa njia yoyote .
Mamake bwana Kipng’etich’s , Naomi Jeptoo, aliyetalakiana na mzee Kibor miaka miwili iliyopita aliunga mkono msimamo wa mwanawe .
Ameongeza kwamba mwili wa mwanawe aliyezikwa katika shamba linalozozaniwa pia unafaa kufukuliwa ili kufanyiwa vipimo .
Bi Jeptoo amesema hadi leo hajaelewa mbona Mzee Kibor alitalakiana naye kwa sababu alikuwa muaminifu kwa Mzee Kibor tangu walipooana mwaka wa 1975.
Amesema iwapo vipimo hivyo vitafanywa kwa njia ya wazi bila muingilio wowote basi maisha ya wanawe yataboreka . amesema la kuficha na anampenda Mzee Kibor licha ya tofauti kati yao .
Mzee Kibor hata hivyo amesema yungali hajaamua wakati na eneo ambapo vipimo hivyo vitafanywa .Kibor alielezea masaibu aliyopitia na Jeptoo na wanawe na hataki uhusiano wowote nao .