‘Tunawadunga maji’ Daktari feki  wa River road  asimulia jinsi ulaghai unavyofanyika kwa  wanawake wanaotaka makalio na vifua vikubwa

Kumekuwa na  ongezeko la hamu ya baadhi ya wasichana na wanawake kutaka kuongeza ukubwa wa matiti na makalio yao ili kuonekana warembo au kuwavutia wanaume  na  kuzua  vuguvugu kubwa la madaktari feki katika eneo la river road hapa jijini Nairobi ambao wapo tayari kuwadunga  sindano  na kemikali wanawake wanaotaka kuafikia maumbo mapya .

Mwanamke  mmoja amekiri kwamba amekuwa akijishughulisha  na biashara  ya kuwadunga dawa wanawake ili waweze kuafikia mahitaji ya wateja hao wao wa kike . Amesema  ‘unapigwa shindano ukiwa ndani ya stall’. Kulingana naye,matibabu hayo bandia na hatari kwa afya hutolewa katika duka zao   na hata kuna wahudumu wanaovalia  aproni za madaktari ilhali hawajahitimu .

Hata hivyo ametoa ufichuzi ambao utawashangaza wengi wakiwemo waliodungwa sindano za kuongeza kiasi cha sehemu wanazotaka Wamekuwa wakidungwa sindano zenye maji na hata sio kemikali  zinazoahidiwa kutumiwa . ‘Kuna wale ambao hata huzirai tukiwadunga, haifanyangi kazi ni maji plain’ amesema .

Kumekuwa na visa vya wanawake na wasichana kukosa kuamini  maombo yao na kufedheheshwa kwamba labda hawavutii jambo ambalo limewatia wengi mashakani kwa kujiingiza katika njia hatari za kujaribu kujibadilisha kimuonekano na kuhatarisha  maisha yao .