Pengo hilo limeacha mwanya wa uwezekano wa DP Ruto kufurushwa kupitia kura ya kutokuwa na imani naye . Hilo limedhihirika baada ya maseneta 54 kupiga kura ya kuidhinisha kuondolewa wa Kindiki Kithure kama naibu wa spika wa senate dhidi ya masenetya saba waliojaribu kuikoa kazi ya Kithure .
Kindiki ambaye ni profesa wa sharia na msomi tajika amekuwa miongoni mwa wafuasi sugu wa Ruto na wanaomuunga mkono kuchukua usukani kutoka kw arais Kenyatta mwaka wa 2022 na kuondolewa kwake kama naibu wa spika kutapiga pancha jitihada na ushaiwishi wake katika eneo la mashariki mwa Mlima Kenya . Kwa wakati mmoja aliwahi kutajwa kama viongozi ambao huenda wakatumiwa na Ruto kama mgombea mwenzake katika uchaguzi mkuu ujao na kuondolewa kwake kutakuwa pigo kwa kambi ya Ruto na kwa taaluma yake kisiasa .
Siku ya ijumaa maseneta 54 kati ya 67 waliidhinisha kura ya kumuondoa kindiki kutoka wadhifa huo .ni saba pekee ambao walipinga kura hiyo na ni Kipchumba Murkomen wa Elgeyo Marakwet, Susan Kihika wa Nakuru, Samson Cherargei wa Nandi, Aaron Cheruiyot wa Kericho, Christopher Lang'at wa Bomet na seneta wa Meru Mithika Linturi. Maseneta wawili ambao waliunga mkono kuondolewa kwa Ruto ingawa hawaku bungeni wangezidisha idadi ya wanaompinga Ruto kuwa 56 lakini kura zao hazikukubalika .
Hoja hiyo ilihitaji tu maseneta 45 ili kupitishwa .
Katika kinachoonekana kama kubadili msimamo wao ,maseneta watano wateule ambaop hapo awali walikuwa katika kambi ya Ruto walimuacha na kupiga kura pamoja na maseneta wa mrengo wa rais Kenyatta na kiongozi wa Odm Raila Odinga ambao waliunda ngome ya pingamizi dhidi ya Ruto .
Maseneta hao ni Falhada Dekow Iman, Naomi Jillo Waqo, Victor Prengei, Mary Seneta Yiane a na Millicent Omanga.