Ligi ya mabingwa Uropa: Man United watashinda?

Klabu mbali mbali kutoka bara Uropa zinatarajiwa kuchuana leo usiku huku wakufunzi wakiwa na imani kuwa wachezaji wao wataweza kuandikisha ushindi ili waweze kufuzu katika ngazi utakaofuata.

Man United vs Partizan

Vijana wake Ole Gunnar Solsjaer watakuwa wanakaribisha klabu ya Partizan uwanjani Old Trafford.

 Man United walipoteza mechi dhidi ya Bounermouth katika ligi ya Uingereza wikendi uliopita na mashabiki wao wanatarajia klabu hio itapata ushindi usiku wa leo.

Klabu ya Partizan kwa sasa wanashikilia nambari tatu wakiwa na pointi 4 katika kundi L, huku Man United wakiwa kileleni na pointi 7.

Utabiri wangu ni Man united watashinda mechi hiyo kwa mabao 3-1.

Roma vs Monchengladbach

 Ni mchuano ambayo klabu ya Roma wanatarajiwa kupata ushindi mkubwa kwani wapo kileleni katika kundi J wakiwa na pointi 5 huku Monchengladbach wakiwa wa mwisho katika kundi hilo na pointi 2.

Utabiri wangu ni Roma itashinda mechi hiyo kwa mabao 4-2.