Gavana Mutua awashutumu viongozi wa Azimio kwa kuwa na kiburi

Muhtasari
  • Alitaja upendeleo wa baadhi ya vyama vya kisiasa katika Azimio na kutengwa kwa MCC
GAVANA WA MACHAKOS ALFRED MUTUA
Image: WILFRED NYANGARESI

Kiongozi wa chama cha Maendeleo Chap Chap Alfred Mutua amewaonya viongozi wa Azimio la Umoja One Kenya Alliance dhidi ya kuwa na kiburi.

Akizungumza wakati wa mahojiano ya runinga ya Citizen mnamo Jumanne, Mutua alisema Azimio haina ufahamu kwa kufikiria wengine hawajali na akapuuzilia mbali madai kwamba hana ushawishi kwa umma.

"Wanafaa kukomesha kiburi hiki cha kudhani kuwa wao ndio pekee wanaodhibiti umma. Ni aina hiyo ya kiburi ambayo imemshuhudia Azimio akitumbukia kwenye mkondo," gavana wa Machakos alisema.

"Kama nisingekuwa na athari, wasingekuwa wanazungumza kunihusu. Wangenipuuza."

Msemaji huyo wa zamani wa Serikali alisema kuwa bado anaweza kuaminiwa na kuthibitisha kwamba amefuata kanuni zake licha ya kuhamia kambi ya Ruto.

" Kwa sababu tu unahamisha nafasi kwa wakati huu kwa sababu kila kitu kinabadilika, haimaanishi kuwa umebadilisha kanuni zako."

Siku ya Jumatatu, Mutua alitangaza kuwa chama chake kilijiunga na Kenya Kwanza cha Naibu Naibu Rais William Ruto siku ya Jumapili.

Alitaja upendeleo wa baadhi ya vyama vya kisiasa katika Azimio na kutengwa kwa MCC.

"Ruto ni mtu mzuri na ataibadilisha nchi hii. Jana usiku tulitia saini mkataba na Kenya Kwanza na hii hapa nakala na tofauti na Azimio, tunajua yaliyomo," aliwaambia waandishi wa habari.