- Ili kutoa shukrani zake, Bahati amewahakikishia mashabiki wake kuwa ataibuka mshindi katika kinyang'anyiro kikali cha kuwania ubunge wa Mathare
Kevin Kioko Bahati sasa ana sababu ya kutabasamu kwani kilio chake hatimaye kimezaa matunda siku chache baada ya kushinda uteuzi wa chama cha Jubilee katika nia ya kuwania kiti cha Ubunge cha Mathare lakini alikuwa baadaye alinyimwa nafasi hiyo.
Mwanamuziki huyo sasa amepata nafasi ya pili na amepewa mwanga wa kugombea nafasi hiyo baada ya cheti cha uteuzi kurejeshwa kwake.
Bahati alipewa tikiti ya kuwania kiti cha ubunge wa Mathare katika hafla iliyohudhuriwa na katibu mkuu wa Chama cha Jubilee Jeremiah Kioni ambaye alibaini kuwa Bahati anawakilisha sura ya vijana anastahili kupata fursa sawa kama Mkenya kuwania kiti hicho.
Ili kutoa shukrani zake, Bahati amewahakikishia mashabiki wake kuwa ataibuka mshindi katika kinyang'anyiro kikali cha kuwania ubunge wa Mathare.
Hatimaye Bahati amevunja ukimya baada ya kutunukiwa tikiti ya kiti cha Ubunge wa Mathare huku akimtumia ujumbe maalum Rais Uhuru Kenyatta. .
Bahati amemshukuru Rais Uhuru kwa kumpa nafasi ya dhahabu na kumwamini.
"Asante Rais Wangu na Kiongozi wa Chama Changu H.E Uhuru Kenyatta kwa nafasi ya kuleta Mabadiliko huko Mathare. Asante pia kwa kuwapa Nafasi Vijana wa Nchi hii Kuleta Mchango wao katika Serikali ya Azimio... Mungu Akubariki Mr President 🙏."