Karua: Kwa nini sitatoka Azimio ikiwa Raila hatanichagua

Muhtasari
  • Kiongozi wa chama cha Narc Kenya, Martha Karua, anasema atashikamana na aliyekuwa Waziri Mkuu, Raila Odinga, hata kama hatachaguliwa kuwa mgombea mwenza wa Azimio One Kenya
Image: Martha Karua/TWITTER

Kiongozi wa chama cha Narc Kenya, Martha Karua, anasema atashikamana na aliyekuwa Waziri Mkuu, Raila Odinga, hata kama hatachaguliwa kuwa mgombea mwenza wa Azimio One Kenya.

Akizungumza katika kaunti ya Mombasa siku ya Jumamosi, Mei 14, Karua alieleza kuwa mahitaji ya Wakenya yalipita yale ya malengo yake ya kisiasa.

Karua, ambaye anachukuliwa kuwa mshiriki wa mbele wa nafasi hiyo, aliongeza kuwa watasalia na umoja hata baada ya Raila kumtaja mgombea mwenza huku wakipigia debe uungwaji mkono kwa Waziri Mkuu huyo wa zamani.

Alitoa kauli hizo baada ya Mwakilishi wa Wanawake wa Murang’a, Sabina Chege, kuwataka wagombeaji waliohojiwa kuwania nafasi hiyo kuunga mkono uwaniaji wa Raila bila masharti yoyote.

"Kama vile Sabina Chege alisema, sisi sote tuliokuwa na nia ya kumrithi Raila tutaambatana naye na kuendelea na kazi yetu. Hakuna atakayeondoka kwa sababu sio matarajio yetu ya kibinafsi bali ya Wakenya," alisema.

Kwa upande wake, Chege alimsuta kiongozi wa Wiper, Kalonzo Musyoka, na timu yake kwa kutoa matamshi, akieleza kuwa chaguo la mwisho litaamuliwa na Raila.

"Nataka kumhakikishia Raila kwamba hatutakulazimisha. Tutaunga mkono uamuzi wako kwa asilimia 100 bila shinikizo lolote. Umenifunza kwa miaka mingi na haijalishi uamuzi wako, nitakuunga mkono.

"Ni uamuzi wako na hakuna mtu anayepaswa kukupa masharti. Kuwa huru kutangaza naibu wako. Wewe ndiye tumaini pekee katika nchi hii," alisema.