DP William Ruto wa kwanza kupiga kura Sugoi

Ruto alifika katika kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi ya Koschei kabla ya saa 6:00 asubuhi

Muhtasari

• Ruto alifika katika kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi ya Koschei kabla ya saa 6:00 asubuhi

DP William Ruto akiwa katika kituo cha piga kura cha Sugoi
DP William Ruto akiwa katika kituo cha piga kura cha Sugoi
Image: screengrab

Naibu Rais William Ruto amempigia kura Sugoi.

Mgombea urais wa Kenya Kwanza alifika katika kituo cha kupigia kura pamoja na mkewe Mama Rachel Ruto.

Maafisa wa IEBC walichukua bayometriki ya DP Ruto kabla ya kupiga kura katika kituo cha Sugoi.

Ruto alifika katika kituo cha kupigia kura cha shule ya msingi ya Koschei akiwa amevalia kawaida.

Wakenya leo wanapiga kura zao katika vituo tofauti vya kupigia kura.