logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jalang'o ajiamini kushinda kinyang'anyiro cha ubunge Lang'ata

Jalang'o alipiga kura katika shule ya msingi ya Uhuru Gardens mapema asubuhi.

image
na Davis Ojiambo

Uchaguzi09 August 2022 - 16:09

Muhtasari


  • •Jalang'o alionyesha imani kuwa atawashinda wapinzani wake katika kinyang'anyiro hicho na kuapishwa kama mbuge wa Langata.
Jalango

Mtangazaji aliyegeuka kuwa mwanasiasa Felix Odiwuor, almaarufu Jalang'o amehutubia wafuasi wake baada ya kujipigia kura.

Mgombea ubunge huyo wa Lang'ata kwa tikiti ya ODM alipiga kura katika shule ya msingi ya Uhuru Gardens mapema asubuhi.

Jalang'o alionyesha imani kuwa atawashinda wapinzani wake katika kinyang'anyiro hicho na kuapishwa kama mbuge wa Langata.

Pia alisema kuwa atatembelea vituo vingine vya kupigia kura ndani ya jimbo hilo ili kuhakikisha wafuasi na maajenti wake wako salama.

''Lazima nitembee niakikishe kwamba agents wangu wako vizuri an taratibu zote zinafuatwa ili kusiwe na hitilafu yeyote. Sisi tuko tayari kufanya kazi na kuhakikisha kwamba tumemaliza vizuri," Alisema.

Mtangazaji huyo wa zamani wa redio pia aliwashukuru mashabiki wake kwa kumuunga mkono hadi mwisho wa safari.

"Tumepiga kura an nimamaliza. Asanteni sana kwa ambao wamekuwa nasi katika hii safari. Haijkuwa safari rahisi, imekuwa safari ndefu na tumemaliza sasa ni kusubiri tu an kuona kuwa tunapata mafanikio," Jalang'o aliongeza.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved