logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Jamaa akamatwa baada ya kupatikana na panga na kisu katika kituo cha kupigia kura Homa Bay

Polisi walimpata mshukiwa walipokuwa wanakagua kituo hicho baada ya shughuli za upigaji kura kukamilika.

image
na SAMUEL MAINA

Uchaguzi09 August 2022 - 15:55

Muhtasari


  • •Mshukiwa alikamatwa Jumanne jioni baada ya kupatikana katika kituo cha kupigia kura cha Shule ya Msingi ya Shauri Yako akiwa amejihami kwa panga na kisu.
  • •Maafisa wa polisi walimpata mshukiwa walipokuwa wanakagua kituo hicho baada ya shughuli za upigaji kura kukamilika.

Polisi katika kaunti ya Homa Bay wanamzuilia mwanaume mmoja aliyepatikana na silaha katika kituo cha kupiga kura.

Mshukiwa alikamatwa Jumanne jioni baada ya kupatikana katika kituo cha kupigia kura cha Shule ya Msingi ya Shauri Yako akiwa amejihami kwa panga na kisu.

Maafisa wa polisi walimpata mshukiwa walipokuwa wanakagua kituo hicho baada ya shughuli za upigaji kura kukamilika.

Baada ya kutiwa pingu mwanaume huyo alizidikishwa hadi kituo cha polisi kwa hatua zaidi kuchukuliwa.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved